Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi afanya mazungumzo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Ikulu, Zanzibar leo tarehe 22 Novemba 2025.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akiwa na Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Hakainde Hichilema pamoja na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Watu wa China Mhe. Li Qiang, wakiweka jiwe la msingi la uzinduzi wa Ukarabati Mkubwa wa Reli ya TAZARA iliyofanyika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mulungushi Jijini Lusaka nchini Zambia. Tarehe 20 Novemba 2025.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akabidhiwa Ofisi ya Makamu wa Rais, Ikulu Chamwino mkoani Dodoma, tarehe 04 Novemba 2025.
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. George Masaju akimuapisha Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika hafla iliyofanyika Uwanja wa Gwaride, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma leo tarehe 03 Novemba 2025.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ashiriki zoezi la kupiga kura ya kuchagua Rais, Mbunge na Diwani akiwa katika Kijiji cha Kasumo, Wilaya ya Buhigwe mkoani Kigoma leo tarehe 29 Oktoba 2025.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ameungana na Viongozi, Waumini pamoja na Wananchi mbalimbali katika Ibada ya kumuombea Baba wa Taifa Hayati Mwalimu. Julius Kambarage Nyerere iliyofanyika katika Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Francisko wa Asizi, Mwanjelwa Mkoani Mbeya tarehe 14 Oktoba 2025. Ibada hiyo imeongozwa na Akofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Mbeya Mhashamu Gervas Nyaisonga.