Maktaba ya Picha

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango amejumuika na viongozi mbalimbali wa Serikali, Dini na Chama katika dua ya pamoja ya kumuombea aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Hayati Sheikh Abeid Amani Karume katika kumbukizi ya miaka 52 ya kifo chake tarehe 07 Aprili 2024 iliyofanyika Afisi Kuu ya Chama Cha Mapinduzi – Kisiwandui Zanzibar.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango ameongoza viongozi na wananchi kuaga mwili wa Waziri Mkuu Mstaafu Hayati Edward Ngoyai Lowassa katika Viwanja vya Karimjee Jijini Dar es salaam tarehe 13 Februari 2024.
Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Mpango amepokea vifaa tiba kwa ajili ya Watoto Njiti kutoka Taasisi ya Doris Mollel na vifaa tiba kutoka Tume ya Taifa ya Ushindani katika Hospitali ya Wilaya ya Buhigwe, Kigoma Julai 06, 2023.
Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Mpango amefungua Hoteli ya Kisasa ya Bwami Dubai iliopo Wilaya ya Kasulu Mkoani Kigoma Julai 05, 2023.
Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Mpango amepokea Madarasa, Samani mbalimbali na Ofisi za Walimu yaliokarabatiwa na Benki ya Biashara Tanzania (TCB) katika Shule ya Msingi Muyama wilayani Buhigwe, Kigoma Julai 05, 2023.
Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Mpango amezindua Tawi la Benki ya NMB Wilaya Buhigwe mkoani Kigoma Julai 04, 2023.
Settings