Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara

Wasiliana na Makamu wa Rais kutumia anwani zifuatazo

PERMANENT SECRETARY
THE OFFICE OF VICE PRESIDENT
GOVERNMENT CITY
P. O. Box 2502,
Dodoma, Tanzania
Tel. No. : + (255) 026 2329006
Fax No. : + (255) 026 2329007/2963150
Email: ps@vpo.go.tz / km@vpo.go.tz

AU

PERMANENT SECRETARY
THE OFFICE OF VICE PRESIDENT
6 Albert Luthuli Street,
P. O. Box 5380,
11406 Dar es Salaam, Tanzania
Tel. No. : + (255) 22 2113857/2116995
Fax No. : + (255) 22 2113856
Email: ps@vpo.go.tz / km@vpo.go.tz

Maeneo ya Muungano yapo 22 kama yalivyoorodheshwa katika nyongeza ya kwanza ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo ni kama yafuatayo:-

1.Katiba ya Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Muungano ;

2.Mambo ya Nchi za Nje ;

3.Ulinzi na Usalama;

4.Polisi;

5.Mamlaka juu ya mambo yanayohusikana na hali ya hatari;

6.Uraia;

7.Uhamiaji;

8.Mikopo na biashara ya Nchi za Nje ;

9.Utumishi katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano;

10.Kodi ya mapato inayolipwa na watu binafsi na mashirika, ushuru wa forodha na ushuru wa
bidhaa zinazotengenezwa Nchini Tanzania unaosimamiwa na Idara ya Forodha;

11.Bandari, mambo yanayohusika na usafiri wa anga, posta na simu;

12.Mambo yote yanayohusika na sarafu, fedha kwa ajili ya malipo yote halali (pamoja na noti),
mabenki ( pamoja na mabenki ya kuweka akiba) na shughuli zote za mabenki;fedha za kigeni na
usimamizi juu ya mambo yanayohusika na fedha za kigeni;

13.Leseni za Viwanda na Takwimu ;

14.Elimu ya Juu;

15.Mahakama ya Rufaa ya Jamhuri ya Muungano ;

16.Maliasili ya Mafuta, pamoja na mafuta yasiyochujwa ya motokaa na mafuta ya aina ya petroli na aina nyinginezo za mafuta au bidhaa, na Gesi asilia ;

17.Baraza la Taifa la Mitihani la Tanzania na mambo yote yanayohusika na kazi za Baraza hilo ;

18.Usafiri na usafirishaji wa anga ;

19.Utafiti;

20.Utabiri wa Hali ya Hewa;

21.Takwimu;na

22.Uandikishaji wa Vyama vya Siasa na mambo mengine yanayohusiana na hayo.

Settings