Habari
Waziri Masauni, Balozi wa Djibouti wateta
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Africa Sovereign Carbon Registry (ASCR) Foundation ya Djibouti, Mhe. Balozi Ahmed Araita, lengo likiwa kuimarisha ushirikiano katika biashara ya kaboni.
Mazungumzo hayo yamefanyika Machi 25,2026 jijini Dodoma ambapo Mhe. Masauni amesema nchi za Afrika zinapaswa kushirikiana katika kukabiliana na mabadiliko tabianchi.
Amesema kuwa hali ya mabadiliko ya tabianchi inapaswa kushughulikiwa haraka huku akisisitiza Waafrika kuzungumza lugha moja na kuweka malengo ya pamoja ili kukabiliana nayo



