Makamu wa Rais awasili Angola kushiriki Mkutano wa SADC

Aug, 16 2023

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango leo tarehe 16 Agosti 2023 amewasili Jijini Luanda nchini Angola ambapo anatarajia kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa 43 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika (SADC) utakaofanyika tarehe 17 Agosti 2023.

Mkutano huo wenye kaulimbiu isemayo “Umuhimu wa Rasilimali Fedha na Rasilimali Watu katika kuendeleza Viwanda na Uchumi” utajadili masuala mbalimbali yahusuyo Jumuiya hiyo.

Aidha, Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali umetanguliwa na mkutano wa Kamati ya Baraza la Mawaziri la Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) uliofanyika tarehe 13–14 Agosti 2023.

Settings