Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Makamu wa Rais

Masauni awaomba wabunge kusahihisha upotoshaji Muungano

Feb, 11 2026

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni ametoa rai kwa wabunge kupinga na kusahihisha upotoshaji wa taarifa kuhusu Muungano, hususan kupitia mikutano ya hadhara na mitandao ya kijamii.

Ametoa rai hiyo wakati wa semina kuhusu Muungano na Mazingira kwa wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyofanyika katika Ukumbi wa Pius Msekwa jijini Dodoma, Februari 11, 2026.

Mhandisi Masauni amesema kuwa Muungano una faida nyingi hivyo ni wakati sasa wabunge kusikiliza na kuwasilisha kwa busara hoja za wananchi kuhusu Muungano

Amesisitiza kuwa wabunge ni nguzo muhimu ya kulinda na kuimarisha Muungano wa Tanzania na wanabeba dhamana ya kihistoria ya kuhakikisha Muungano unaendelea kuwa chanzo cha amani, mshikamano na maendeleo ya Taifa.

Kwa upande wa mazingira, amesema Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kushirikiana na wadau imeandaa Programu ya Mageuzi ya Kukijanisha Tanzania ikiwa na lengo la kuleta mageuzi jumuishi na shirikishi yenye matokeo makubwa yanayolenga kuimarisha uhimilivu wa mabadiliko ya tabianchi kwa kuongeza eneo lenye uoto wa kijani kupitia upandaji miti.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira Mhe. Jackson Kiswaga amesema kupitia semina hiyo wamepata uelewa mklubwa kuhusu masuala ya mazingira.

Ameahidi kuwa pamoja na wabunge wenzao wataendelea kuwa mabalozi wazuri kwa wananchi katika kuwafundisha kuhusu uhifadhi wa mazingira endelevu.

Habari

Masauni awaomba wabunge kusahihisha upotoshaji Muungano


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni ametoa rai kwa wabunge kupinga na kusahihisha upotoshaji wa taarifa kuhusu Muungano, hususan kupitia mikutano ya hadhara na mitandao ya kijamii.

Ametoa rai hiyo wakati wa semina kuhusu Muungano na Mazingira kwa wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyofanyika katika Ukumbi wa Pius Msekwa jijini Dodoma, Februari 11, 2026.

Mhandisi Masauni amesema kuwa Muungano una faida nyingi hivyo ni wakati sasa wabunge kusikiliza na kuwasilisha kwa busara hoja za wananchi kuhusu Muungano

Amesisitiza kuwa wabunge ni nguzo muhimu ya kulinda na kuimarisha Muungano wa Tanzania na wanabeba dhamana ya kihistoria ya kuhakikisha Muungano unaendelea kuwa chanzo cha amani, mshikamano na maendeleo ya Taifa.

Kwa upande wa mazingira, amesema Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kushirikiana na wadau imeandaa Programu ya Mageuzi ya Kukijanisha Tanzania ikiwa na lengo la kuleta mageuzi jumuishi na shirikishi yenye matokeo makubwa yanayolenga kuimarisha uhimilivu wa mabadiliko ya tabianchi kwa kuongeza eneo lenye uoto wa kijani kupitia upandaji miti.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira Mhe. Jackson Kiswaga amesema kupitia semina hiyo wamepata uelewa mklubwa kuhusu masuala ya mazingira.

Ameahidi kuwa pamoja na wabunge wenzao wataendelea kuwa mabalozi wazuri kwa wananchi katika kuwafundisha kuhusu uhifadhi wa mazingira endelevu.

Settings