Habari
Makamu wa Rais ashiriki uapisho wa Viongozi Ikulu Zanzibar
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi ameshiriki uapisho wa Wakuu wa Mikoa wanne na Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani, walioapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika hafla iliyofanyika Ikulu Ndogo – Tunguu Zanzibar leo tarehe 02 Septemba 2026.
Viongozi walioapishwa ni pamoja na Mhe. CP Salum Rashid Hamduni, kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Alexander Pastory Mnyeti kuwa Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Stanslaus Haroon Nyongo kuwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani na Mhe. Jumanne Abdallah Sagini, kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya.
Aidha, Ndg. Richard Marcellino Kayombo ameapishwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani.



