Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Makamu wa Rais

Makamu wa Rais ashiriki uapisho wa Viongozi Ikulu Zanzibar

Sep, 02 2026

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi ameshiriki uapisho wa Wakuu wa Mikoa wanne na Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani, walioapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika hafla iliyofanyika Ikulu Ndogo – Tunguu Zanzibar leo tarehe 02 Septemba 2026.

Viongozi walioapishwa ni pamoja na Mhe. CP Salum Rashid Hamduni, kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Alexander Pastory Mnyeti kuwa Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Stanslaus Haroon Nyongo kuwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani na Mhe. Jumanne Abdallah Sagini, kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya.

Aidha, Ndg. Richard Marcellino Kayombo ameapishwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani.

Habari

Makamu wa Rais ashiriki uapisho wa Viongozi Ikulu Zanzibar


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi ameshiriki uapisho wa Wakuu wa Mikoa wanne na Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani, walioapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika hafla iliyofanyika Ikulu Ndogo – Tunguu Zanzibar leo tarehe 02 Septemba 2026.

Viongozi walioapishwa ni pamoja na Mhe. CP Salum Rashid Hamduni, kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Alexander Pastory Mnyeti kuwa Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Stanslaus Haroon Nyongo kuwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani na Mhe. Jumanne Abdallah Sagini, kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya.

Aidha, Ndg. Richard Marcellino Kayombo ameapishwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani.

Settings