Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Makamu wa Rais

Waziri Masauni afungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya Makamu wa Rais

Apr, 15 2026
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amesema Mikutano ya Baraza la Wafanyakazi ni nyenzo muhimu ya kujadili utekelezaji wa majukumu, kubaini changamoto na kuweka mikakati ya kuboresha utendaji kwa kuzingatia misingi ya uwajibikaji na weledi.

Amesema ili kuendelea kuboresha utendaji kazi na kuongeza ufanisi na tija katika utekelezaji wa majukumu, ni muhimu kudumisha utamaduni wa kufanya kazi kwa umoja, bidii na weledi. Tunapaswa kujipambanua kwa utendaji wa hali ya juu unaoendana na hadhi ya Ofisi ya Makamu wa Rais katika nchi.

Mhe. Masauni ameyasema hayo wakati akifungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya Makamu wa Rais uliofanyika Dodoma, Aprili 15, 2026 akieleza kuwa Ofisi imeendelea kufanya vizuri katika kudumisha Muungano, hususan kupitia utoaji wa elimu kwa umma kwa makundi mbalimbali.

“Kwa upande wa usimamizi wa mazingira, Ofisi imefanikiwa kufanya marekebisho ya Sheria ya Usimamizi wa Mazingira, Sura 191, hususan kwa kuimarisha vifungu vinavyohusu mabadiliko ya tabianchi na kuanzisha Kituo cha Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC).

Aidha, ni muhimu kuendelea kuimarisha uwezo wa kitaalam na kitaasisi, upatikanaji wa rasilimali na kuongeza jitihada za uhamasishaji wa rasilimali fedha, ikiwemo kupitia maandalizi bora ya miradi ya uhifadhi wa mazingira.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya Makamu wa Rais ambaye pia Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi alisema lake kuu tangu kuanzishwa kwake baraza hilo lilikuwa kuimarisha ushirikishwaji wa wafanyakazi katika kupanga, kutekeleza na kutathmini mipangokazi, pamoja na kuboresha uhusiano kati ya Menejimenti na watumishi.

“Madhumuni ya Mkutano huu ni kuwashirikisha wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Rais kwa lengo la kupata Taarifa ya utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Ofisi.”

Habari

Waziri Masauni afungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya Makamu wa Rais


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amesema Mikutano ya Baraza la Wafanyakazi ni nyenzo muhimu ya kujadili utekelezaji wa majukumu, kubaini changamoto na kuweka mikakati ya kuboresha utendaji kwa kuzingatia misingi ya uwajibikaji na weledi.

Amesema ili kuendelea kuboresha utendaji kazi na kuongeza ufanisi na tija katika utekelezaji wa majukumu, ni muhimu kudumisha utamaduni wa kufanya kazi kwa umoja, bidii na weledi. Tunapaswa kujipambanua kwa utendaji wa hali ya juu unaoendana na hadhi ya Ofisi ya Makamu wa Rais katika nchi.

Mhe. Masauni ameyasema hayo wakati akifungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya Makamu wa Rais uliofanyika Dodoma, Aprili 15, 2026 akieleza kuwa Ofisi imeendelea kufanya vizuri katika kudumisha Muungano, hususan kupitia utoaji wa elimu kwa umma kwa makundi mbalimbali.

“Kwa upande wa usimamizi wa mazingira, Ofisi imefanikiwa kufanya marekebisho ya Sheria ya Usimamizi wa Mazingira, Sura 191, hususan kwa kuimarisha vifungu vinavyohusu mabadiliko ya tabianchi na kuanzisha Kituo cha Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC).

Aidha, ni muhimu kuendelea kuimarisha uwezo wa kitaalam na kitaasisi, upatikanaji wa rasilimali na kuongeza jitihada za uhamasishaji wa rasilimali fedha, ikiwemo kupitia maandalizi bora ya miradi ya uhifadhi wa mazingira.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya Makamu wa Rais ambaye pia Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi alisema lake kuu tangu kuanzishwa kwake baraza hilo lilikuwa kuimarisha ushirikishwaji wa wafanyakazi katika kupanga, kutekeleza na kutathmini mipangokazi, pamoja na kuboresha uhusiano kati ya Menejimenti na watumishi.

“Madhumuni ya Mkutano huu ni kuwashirikisha wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Rais kwa lengo la kupata Taarifa ya utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Ofisi.”
Settings