Makamu wa Rais awaagiza MaDC kutumia magari kutatua changamoto

Jul, 09 2024

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amewaagiza Wakuu wa Wilaya pamoja na viongozi kwa ujumla kutumia magari wanayokabidhiwa kwa kufanya kazi za wananchi ikiwemo kuwatembelea na kutatua changamoto zinazowakabili.

Makamu wa Rais amesema hayo wakati akikabidhi magari matano kwa Wakuu wa Wilaya Tano za Mkoa wa Kigoma akiwa ziarani mkoani humo. Amesema bado utekelezaji wa agizo lililotolewa kwa viongozi kuwatembelea wananchi katika maeneo yao halitekelezwi kikamilifu.

Aidha amewasihi viongozi hao kutunza magari na kuyatumia kwa matumizi sahihi ikiwemo kufuata maadili ya utumishi wa umma. Ameagiza magari hayo kutotumika vibaya na kuonekana katika maeneo ya starehe. Amesema magari hayo yanapaswa kuwa chachu ya kuwatembelea wananchi kwa kasi zaidi.

Settings