Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Makamu wa Rais

Makamu wa Rais ashiriki Misa ya kuwekwa wakfu Askofu Msaidizi Dar

Sep, 05 2026

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi ameshiriki Adhimisho la Misa Takatifu ya kuwekwa Wakfu Mhashamu Vincent Mpwaji, kuwa Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, iliyofanyika katika Viwanja vya Msimbazi Center – Dar es Salaam, leo tarehe 05 Septemba 2026.

Misa hiyo, imeongozwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam Mhashamu Jude Thaddeus Ruwa’ichi, ambaye ni Askofu kiongozi katika uwekaji Wakfu, akisaidiwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dodoma Mhashamu Beatus Kinyaiya pamoja na Askofu Msaidizi Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam Mhashamu Henry Mchamungu.

Pia, Adhimisho hilo limehudhuriwa na Maaskofu kutoka Majimbo Katoliki mbalimbali nchini, Viongozi wa madhehebu mbalimbali ya Kikristo, Viongozi wa Serikali, Viongozi wa Taasisi, Mapadre, Watawa, familia, ndugu, marafiki pamoja na waumini kutoka maeneo mbalimbali.

Habari

Makamu wa Rais ashiriki Misa ya kuwekwa wakfu Askofu Msaidizi Dar


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi ameshiriki Adhimisho la Misa Takatifu ya kuwekwa Wakfu Mhashamu Vincent Mpwaji, kuwa Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, iliyofanyika katika Viwanja vya Msimbazi Center – Dar es Salaam, leo tarehe 05 Septemba 2026.

Misa hiyo, imeongozwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam Mhashamu Jude Thaddeus Ruwa’ichi, ambaye ni Askofu kiongozi katika uwekaji Wakfu, akisaidiwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dodoma Mhashamu Beatus Kinyaiya pamoja na Askofu Msaidizi Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam Mhashamu Henry Mchamungu.

Pia, Adhimisho hilo limehudhuriwa na Maaskofu kutoka Majimbo Katoliki mbalimbali nchini, Viongozi wa madhehebu mbalimbali ya Kikristo, Viongozi wa Serikali, Viongozi wa Taasisi, Mapadre, Watawa, familia, ndugu, marafiki pamoja na waumini kutoka maeneo mbalimbali.

Settings