Kitengo cha Huduma za Sheria
            
                            Kitengo kinaongozwa na Mkurugenzi

Bw. Dustan Shimbo
Lengo
Kutoa utaalamu wa huduma za kisheria katika Ofisi
Kitengo kinatekeleza majukumu kama ifuatavyo:-
- (i)            Kutoa msaada wa kisheria kwa Ofisi na Taasisi zake katika kutafsiri sharia, na makubaliano mengine ya kisheria; 
 - (ii)           Kutoa ushauri wa kitaalamu katika maandalizi ya nyaraka za kisheria kwa kushirikiana na Ofisi ya Mwakasheria Mkuu wa Serikali;
 - (iii)         Kuchambua na kushauri kuhusu sharia, kanuni na miongozo inayohusu masuala ya Muungano na yasio ya Muungano;(iv)         Kushiriki katika mashauriano na mikutano ya kisheria inayohusu Mazingira, Muungano na masuala yasiyo ya Muungano;
 -   (v)           Kutafsiri sheria kuhusu masula ya Mazingira; 
 - (vi)         Kusikiliza mashauri ya jinai na madai yanayohusu Ofisi kwa kushirikiana na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali; na (vii)       Kufuatilia, kutathmini na kutoa taarifa ya utekelezaji wa maamuzi ya mahakama kuhusu mashauri yanayohusu Ofisi katika masuala ya Muungano na yasiyo ya Muungano.