Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Makamu wa Rais

Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara

Wasiliana na Makamu wa Rais kutumia anwani zifuatazo

PERMANENT SECRETARY
THE OFFICE OF VICE PRESIDENT
GOVERNMENT CITY
P. O. Box 2502,
Dodoma, Tanzania
Tel. No. : + (255) 026 2329006
Fax No. : + (255) 026 2329007/2963150
Email: ps@vpo.go.tz / km@vpo.go.tz

AU

PERMANENT SECRETARY
THE OFFICE OF VICE PRESIDENT
6 Albert Luthuli Street,
P. O. Box 5380,
11406 Dar es Salaam, Tanzania
Tel. No. : + (255) 22 2113857/2116995
Fax No. : + (255) 22 2113856
Email: ps@vpo.go.tz / km@vpo.go.tz

Maeneo ya Muungano yapo 22 kama yalivyoorodheshwa katika nyongeza ya kwanza ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo ni kama yafuatayo:-

1.Katiba ya Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Muungano ;

2.Mambo ya Nchi za Nje ;

3.Ulinzi na Usalama;

4.Polisi;

5.Mamlaka juu ya mambo yanayohusikana na hali ya hatari;

6.Uraia;

7.Uhamiaji;

8.Mikopo na biashara ya Nchi za Nje ;

9.Utumishi katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano;

10.Kodi ya mapato inayolipwa na watu binafsi na mashirika, ushuru wa forodha na ushuru wa
bidhaa zinazotengenezwa Nchini Tanzania unaosimamiwa na Idara ya Forodha;

11.Bandari, mambo yanayohusika na usafiri wa anga, posta na simu;

12.Mambo yote yanayohusika na sarafu, fedha kwa ajili ya malipo yote halali (pamoja na noti),
mabenki ( pamoja na mabenki ya kuweka akiba) na shughuli zote za mabenki;fedha za kigeni na
usimamizi juu ya mambo yanayohusika na fedha za kigeni;

13.Leseni za Viwanda na Takwimu ;

14.Elimu ya Juu;

15.Mahakama ya Rufaa ya Jamhuri ya Muungano ;

16.Maliasili ya Mafuta, pamoja na mafuta yasiyochujwa ya motokaa na mafuta ya aina ya petroli na aina nyinginezo za mafuta au bidhaa, na Gesi asilia ;

17.Baraza la Taifa la Mitihani la Tanzania na mambo yote yanayohusika na kazi za Baraza hilo ;

18.Usafiri na usafirishaji wa anga ;

19.Utafiti;

20.Utabiri wa Hali ya Hewa;

21.Takwimu;na

22.Uandikishaji wa Vyama vya Siasa na mambo mengine yanayohusiana na hayo.

Settings