 |
Total site visits: 282742.
|  |
Listed below are the latest items of news:
MAKAMU WA RAIS ZIARANI MKOA WA PWANI
Makamu wa Rais awasili Utete- Makao Makuu ya Wilaya ya Rufiji, Mkoa wa Pwani Januari 01, 2012. Posted:
8th Feb 12
Balozi waNorway nchini akutana na Makamu wa Rais
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Balozi wa Norway nchini Tanzania, Ingunn Klepsivik, wakati alipofika Ofisini kwake Ikulu Dar es Salaam leo Februari 7, 2012 kwa mazungumzo. Picha na Muhidin Sufiani-OMR Posted:
9th Feb 12
Dkt. Ghalib Bilal, Makamu wa Rais akutana naMtafiti bingwa wa Masokwe Duniani
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal na mkewe Mama Asha Bilal, wakizungumza na Mtafiti bingwa wa Masokwe Duniani, aliyekaa nchini kwa miaka 50 akifanya utafiti wa Masokwe katika Mapori ya Gombe na Mahale, Jane Goodall, wakati alipofika Ikulu ndogo Wilaya ya Mpanda mkoa wa Katavi kwa ajili ya mazungumzo jana Februari 18, 2012. Posted:
20th Feb 12
Katibu Mkuu OMR atembelea ukuta wa pangani Tanga
Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais Bw.Sazi Salula (wa tatu kushoto) akitoa Maelekezo kuhusu Ukuta wa Ukingo wa Bahari ya Hindi huko Pangani Tanga wakati wa Ziara yake jana kufuatilia Maagizo ya Makamu wa Rais Dkt Muhammed Gharib Bilali alipofanya ziara hivi hivi karibuni Mkoa wa Tanga. Posted:
10th Feb 12
Kuapishwa kwa balozi wa Tanzania nchini Italia
Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Mhe. James Msekela, anayekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, akati wa hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam leo Februari 7,2012.
Posted:
9th Feb 12
MAKAMU WA RAIS ATUA MKOA WA KATAVI KWA ZIARA YAKE
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwasili kwenye uwanja wa ndege wa Katavi Mkoa wa katavi kwa ajili ya kuanza ziara yake ya siku tatu ya mkoa huo leo Februari 18, 2012. Kushoto ni Mkewe Mama Asha Bilal, na (kulia) ni Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Eng. Stella Manyanya. Picha na Muhidin Sufiani-OMR Posted:
20th Feb 12
Makamu wa Rais ziarani Mkoa wa Pwani
Makamu wa Rais azindua Kambi ya Vijana 400 Wajasiliamali kujifunza utengenezaji wa vigae na ujenzi wa nyumba za bei nafuu. Posted:
9th Feb 12
Mhe. Makamu wa Rais Dkt. Gharib Bilal akitembelea Shamba la Mahindi Mkoani Matavi
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitembelea shamba la mahindi la Waziri Mkuu Mizengo Pinda, lililopo Kijiji cha Vilolo wakati akiwa katika ziara yake ya mkoa wa Katavi na Rukwa leo Februari 20, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR Posted:
20th Feb 12
Mhe. Rais Dkt. Jakaya Kikwete arejea nchini
Rais Jakaya Mrisho Kikwete apokewa na Makamu wa Rais alipowasili akitokea Addis Ababa Ethiopia. Posted:
8th Feb 12
Ushirikiano Mapambano dhidi ya Maharamia
Rais Jakaya Kikwete na Makamu wake washuhudia utiaji saini mkataba wa Ushirikiano katika mapambano dhidi ya Maharamia. Posted:
9th Feb 12
Warsha-Elimu ya Uzalishaji na Matumizi Endelevu
Mkurugenzi Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu OMR afungua Warsha ya Elimu ya Uzalishaji na Matumizi Endelevu. Posted:
8th Feb 12
Waziri Samia Suluhu Hasan atembelea Miradi ya Maendeleo Zanzibar
Katibu wa Kampuni ya Ukweli ni Njia Safi Bi Safia Hashim (Kulia) akimwonesha kito (Lulu), Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano, Mhe Samia Suluhu Hassan,kito ambacho hutumika kutengeneza Pete, alipotembelea kikundi cha akini mama cha Bweleo Wilaya ya Magharibi Unguja wakati wa Ziara yake yakagua Miradi ya Maendeleo ya [TASAF][Picha na Ali Meja} Posted:
22nd Feb 12
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano Samia Suluhu Hassani akiwa Ziarani Zanzibar
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano Samia Suluhu Hassani akitembelea Ujenzi wa Jengo la chuo cha Taasisi ya Sayansi ya Bahari kilichopo Chukwani Wilaya ya Magharibi Mkoa wa Mjini Unguja, Kulia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Sayansi za Bahari Dk Margareth Kyewalyanga[Picha na Ali Meja]
Posted:
22nd Feb 12
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano, Samia Suluhu Hassani akiwa Ziarani Zanzibar
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Muugano Samia Suluhu Hassan akipata Maelezo kutoka kwa Bi Mwajuma Mwinyi (Kulia) kuhusu Matumizi ya Mwani ambao hutengenezwa Sabuni ya Kukogea wakati wa Ziara yake huko BweleoWilaya ya Magharibi Mjini Unguja[Picha na Ali Meja] Posted:
22nd Feb 12
Zawadi ya Kitabu toka kwa Jane Goodall
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea zawadi ya kitabu cha mtafiti bingwa duniani wa Masokwe, Jane Goodall, aliyefika Ikulu ndogo ya Wilaya ya Mpanda mkoa wa Katavi jana Februari 18, 2012 kwa ajili ya mazungumzo. Jane amekaa nchini kwa miaka 50 akifanya utafiti katika mapori ya Gombe na Mahale yaliyopo mkoa wa Kigoma na Katavi. Posted:
20th Feb 12
Ziara Katibu Mkuu wa OMR Pangani Tanga
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bw.Sazi Salula akizungumza na Mmiliki wa Redio Pangani Dkt Vera Pieroth alipotembelea Redio hiyo wakati wa Ziara yake katika Ukuta wa Ukingo wa Bahari Pangani.[Picha na Ali Meja] Posted:
16th Feb 12
Ziara ya Makamu wa Rais mkoani Katavi
Makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Baba mzazi wa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Exavery Kayanza Pinda, wakati alipokuwa akipita kuelekea Kijiji cha Mwamapuli akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Katavi leo, Februari 20. 2012. Kulia nia Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Eng. Stella Manyanya. Picha na Muhidin Sufiani-OMR Posted:
20th Feb 12
Ziara ya Makamu wa Rais mkoani Katavi
Makamu Wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Mohammed Gharib Bilal na mkewe Mama Asha Bilal, wakiwa na mavazi ya asili ya kabila la Kikonongo baada ya kuvishwa na kutunukiwa uchifu wa Kabila la
Kikonongo na machifu wa Kijiji cha Inyonga Wilaya ya Mpanda wakati akiwa katika ziara yake ya mkoa wa Rukwa na Katavi jana Februari 19, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR Posted:
20th Feb 12
Ziara ya Makamu wa Rais mkoani Rukwa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Mkazi wa Kijiji cha Mwamapuli, Yacoub Jilala, ambaye ni mlemavu, baada ya kumaliza kuwahutubia wananchi wa kijiji hicho, alipofika kuzindua jengo la Ghara la mazao, akiwa katika ziara yake ya mkoa wa Rukwa na Katavi, juzi Februari 20, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR Posted:
22nd Feb 12
Ziara ya Makamu wa Rais mkoani Ruvuma
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Askofu wa Jimbo la Katoliki (W) Mbinga, John Ndimbo, wakati alipofika katika Kanisa Kuu la Katoliki Mtakatifu Kiliani, kwa ajili ya kufanya majumuisho baada ya kumazliza ziara yake ya mkoa huo jana Februari 17, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Posted:
20th Feb 12
Ziara ya Makamu wa Rais wilayani Mpanda
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwahutubia wananchi wa Wilaya ya Mpanda Mkoa mpya wa Katavi, wakati alipofika wilaya hiyo kuanza ziara ya mkoa mpya wa Katavi na Rukwa jana, Februari 18, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR Posted:
20th Feb 12
Ziara ya Makamu wa Rais wilayani Nkasi
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikata utepe kuzindua rasmi jengo la Daharia la Shule ya Sekondari ya wasichana ya Korongwe Beach , iliyopo Wilaya ya Nkasi, wakati akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Rukwa na Katavi, jana Februari 21, 2012. Kulia kwake ni
mkewe Mama Asha Bilal. Picha na Muhidin Sufiani-OMR Posted:
22nd Feb 12
Ziara ya Mhe. Dkt Gharib Bilal Mkoani Ruvuma
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Mjiologia Mkuu wa Kampuni ya Mantra Tanzania, Emmanuel Nyamusika kuhusu utafiti wa upatikanaji wa madini ya Urani, wakati Makamu akiwa kazitika ziara yake ya Mkoa wa Ruvuma jana Februari 15, alipotembelea mradi wa Mto Mkuju unaojiandaa na uchimbaji wa madini ya Urani kupitia kampuni yake ya Manta Tanzania.Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Posted:
20th Feb 12
|
|
|
|  |